Macho ya mzee Ismaili yalipomtazama Alice, alihisi miguu yake ikilegea. Picha za siku za nyuma zilianza kumiminika akilini mwake kama maji yanayotiririka mtoni. Alijikuta akitumbua macho kwa
mshangao, huku mapigo ya moyo wake
yakiongezeka kasi.
“Huyu msichana… mbona siwezi kusahau sura yake? ” mzee Ismaili alijiuliza kimoyomoyo, akijaribu kuunganisha matukio
siku mbili zilizopita, baada ya rafiki wa Kelvin, Emanuel, na familia yake kuuawa kikatili, maisha ya Kelvin yalikuwa yamevunjika vipande vipande. Kila mtu kijijini alimwona kijana huyo kama mwenye bahati mbaya, huku wengi wakimkimbia kana kwamba alikuwa laana. Ilikuwa ni mzee Ismaili pekee
aliyemchukua Kelvin na kumpa mahali pa
kuishi.
Lakini ukweli ulikuwa tofauti kabisa.
Kabla Kelvin hajaletwa nyumbani kwake Alice, alikuwa amemtembelea usiku wa manane. Alionekana kana kwamba alikuwa ametoka baharini moja kwa moja, akiwa na mavazi yale yale ambayo alivaa siku alipomtoa kelvim , sku ilipoungua nyumba yake na nguo hizo zilikywa na harufu sans chumvi ya bahari.Hivyo ilikuwa rahisi kwa yule mzee kugundua kuwa yule binti ametoka bahari na nikiumbe wa ajabu ……..
“Nataka Kelvin awe na mahali pa kuishi,
mbali na machungu yote ya yaliyompata,” Alice alimwambia kwa sauti ya upole lakini iliyojaa amri
Mzee Ismaili, akiwa na mshangao, aliuliza, “Kwa nini nisimwambie Kelvin wewe ndo umemsaidia ?”
Alice alimtazama kwa macho makali, akasema, “Hapana. Usitaje jina langu kamwe. Mwambie tu umeamua kumsaidia kwa huruma zako. Ondoa wasiwasi, hii ni siri yangu na yako tu .”
Kwa muda mrefu, mzee Ismaili alihisi hatia
moyoni mwake kila alipomwona Kelvin, akijua kwamba msaada aliompa kijana huyo haukuwa wa huruma zake peke yake, bali ulikuwa mpango wa Alice. Na sasa, siku mbili baadaye , Alice alisimama mbele yake tena.
“Mbona amerudi? Na kwa nini sasa?” mzee Ismaili alijiuliza, akihisi hofu na msisimko wa ajabu.
Alice, akitabasamu kana kwamba hajuwi kitu , alimkaribia mzee huyo na kusema kwa sauti ya utulivu, “Babu, shikilia ile siri
yako na usiseme . Kila kitu bado hakijafika
mwisho.”
Maneno hayo yalimtikisa mzee Ismaili, akajua kwamba Alice ni zaidi ya kiumbe alichowahi kukiona na kitu kilichomchanganya zaidi ni kwamba Alice ana moango gani na kelvin ……
Alice alimtazama mzee Ismaili kwa macho makali yaliyojaa onyo na utulivu wa ajabu. “Nakusihi tena, jifanye hunijui. Kelvin hatakiwi kujua kuwa nilihusika. Wewe ni shujaa wake, si mimi.” nataha hii ibaki kichwani mwake hakuna haja ya kumwambia ata kidogo ……
Mzee Ismaili alijikuta akitikisa kichwa kwa
aibu na hofu. Kabla hajapata nafasi ya kuuliza chochote zaidi, mlango chumba cha kelvin ulifunguliwa taratibu, na Kelvin akaonekana akitoka nje.
Unajua wanaume wengi wale mabachelor wavivu sana kufanya usafi yaani mpaka waje wageni sasa ndo alichokifanya kelvin duuuuuh kazi ya kelvin kuvua samaki kufanya usafi aaaaaaaaaaaaah ………
Kelvin alimtazama Alice, alitabasamu, lakini macho yake yalipogeuka kwa mzee Ismaili, yalijaa shukrani kubwa.
Akamsogelea mzee huyo na kusema kwa
sauti iliyojawa na heshima:
“Babu, huyu ndiye yule msichana niliyekuambia. Lakini ningependa kwanza nikushukuru tena. Wewe ni zaidi ya malaika kwangu. Bila wewe, sijui ningekuwa wapi leo.”
Alice alibaki kimya, akijificha nyuma ya tabasamu la kawaida, huku akiona jinsi Kelvin alivyomsifia mzee Ismaili.
“Huyu mzee alinichukua wakati kila mtu alipoacha kunijali,” Kelvin aliendelea, huku sauti yake ikitetemeka kwa hisia. “Hakika Mungu anakupenda sana, babu.”
Mzee Ismaili alihisi shingo yake ikilowa
jasho. Alikuwa anataka kusema ukweli, kwamba msaada huo ulikuwa umetoka kwa Alice, lakini maneno ya msichana huyo bado yalirindima akilini mwake:
“Jifanye kama hunijuwi na huo msaada umetoa wewe na sio mimi sawa ??.” maneno haya yalumfanya mzee Ismaili ajichukulie ujiko kwa kelvin ningekuwa mimi ilikuwa nafasi ya kutamba huyu mzee ismail anataka kusema nini apunguze kimdomo domo …….
Alice aliingilia kati kwa upole, akisema kwa sauti ya upole, “Kelvin, ni kweli, babu yako ni mtu wa kipekee. Anapaswa kuwa
mfano wa jinsi wanadamu wanavyopaswa
kusaidiana.”
Kelvin alitikisa kichwa kwa kukubaliana, akitabasamu kwa furaha isiyo na kipimo. Hakujua kwamba kati ya Alice na mzee Ismaili kulikuwa na siri nzito ambayo bado yeye haitambuwi kuwa malaika mlinzi kwake ni Alice na sio Mzee Ismail …… yaaani bombooooclaaaaaaaaa mzeee ismail ni ujiko tu yaani bora alimchagua mzee angekuwa kijana tu na kwa binadamu navowajuwa ni kujichukulia sifa tu yaaani mtu yuko tayari akudhalilishe ili yeye asifiwe daaaah binadamu bhana ndo maana hata hamonize alisema ni bora ugali dagaa
kwenye amani ila kuliko wali nyama vitani.
Ila mim nataka hizo nyama na wali huko huko vitani . tuendelee
Baada ya muda mfupi wa mazungumzo ya kawaida, Kelvin alirudi ndani ya nyumba kumpatia mzee Ismaili kikombe cha chai alichokuwa amemwandalia. Alice alipobaki peke yake na mzee huyo, baada ya kelvin kuingia ndani , alisogea karibu na kumwambia kwa sauti ya chini:
“Hakikisha unaficha hadithi hii. Usiharibu imani yake kwako. Wakati ukifika, kila kitu kitakuwa wazi ,hivyo kuwa na amani kelvin
.”
Mzee Ismaili alimtazama Alice kwa macho
ya maswali, lakini msichana huyo alikuwa tayari ameanza kutembea kuelekea nyumbani kwa kelvin Alitembea pole pole huku mzee ismail akimsindikiza kwa macho tu.
MDA KAMA WA DAKIKA TANO BAADAYE….
Alice alikuwa ameketi kitandani, akionekana mwenye utulivu lakini akiwaza kwa undani. Kelvin alipokuwa akipika , alimuomba msaada.
“Alice, nisaidie kuwasha gesi. Nakwenda kuchukua nyanya haraka. sokoni sikujuwa kama ziliisha ….. narudi sasa hivi sawa
???????
Alice alitikisa kichwa kwa kukubaliana,
lakini ndani ya nafsi yake alihisi hofu. Yeye hakuwa binadamu wa kawaida; yeye ni binti nguva, kiumbe wa baharini, asiyejua shughuli za maisha ya kibinadamu.
Kelvin alipokuwa ametoka, Alice alisimama na kusogea karibu na jiko la gesi. Aliangalia kitufe cha gesi kwa udadisi, kisha akajaribu kukizungusha, lakini hakukuwa na mabadiliko. Alijaribu tena, lakini hakuna kitu kilichotokea. Akawa anajitahidi, akihisi huzuni na wasiwasi.
Kwa haraka, aliamua kumuita mzee Ismaili
aliyekuwa karibu nje ya nyumba. “Babu! Tafadhali njooni haraka!”
Mzee Ismaili alisikia sauti yake na kuingia ndani akiharakisha. “Kuna nini, binti?” aliuliza kwa sauti ya upole.
Alice akamwonyesha jiko la gesi. “Babu, siwezi kuwasha moto. Kelvin akirudi ataniona wa ajabu sana.” na hiki sijuwi ni kinini yaaani hata hakizunguki tatizo kwetu havipo ….
Mzee Ismaili alimtazama Alice kwa mshangao, lakini hakusema chochote.
Binti yangu gas unawasha hivi sawa?
Alichukua kiberiti na kuwasha gesi kwa urahis
Alice alicheka na kusema”kumbe rahisi yaani huu ushamba mimi jasho lilikuwa linatiririka kama napigana hivi “
Mzee Ismail alicheka na Alipomaliza, alitenga sufuria na kumwambia Alice:
“Sasa unachotakiwa kufanya ni kukoroga uji huu ili tutengeneze ugali.”
Alice alichukua mwiko kwa tahadhari, lakini mikono yake ilikuwa haina uzoefu kabisa. Alikoroga vibaya, na unga ulikuwa ukitapaka kila mahali. Mzee Ismaili
alicheka kidogo, lakini aligundua hofu
machoni mwa Alice.
“Binti, acha nikuonyeshe. Tunafanya hivi.” Alisema huku akichukua mwiko na kuanza kukoroga kwa ustadi wa ajabu, akipindua uji kwa haraka na kwa usahihi. Alice alimtazama kwa mshangao, akijaribu kujifunza lakini bado akihisi kutokuwa na msaada.
Baada ya kumaliza kusonga ugali, mzee Ismaili alimwambia kwa sauti ya pole:
“Usijali, Alice. Jifunze kidogo kidogo. Kelvin hatagundua lolote.”
Alice alimsifu kwa kumsaidia, na kabla
Kelvin hajarejea, mzee Ismaili alitoweka haraka, akiacha Alice akiendelea kujifanya kana kwamba alimaliza kila kitu peke yake. Kelvin aliporudi, alikuta ugali ukiwa tayari.
Kelvin alisema kwa tabasamu:
“Alice, umefanya kazi nzuri sana. Nashukuru kwa msaada wako.”
Alice alijibu kwa tabasamu la aibu, lakini ndani yake alihisi hatia kwa kutojua hata kazi rahisi kama hiyo. Alijua kwamba hawezi kuficha ukweli wake milele, na kwamba siku moja Kelvin angelazimika kugundua siri yake kubwa.
UPANDE WA BAHARINI NYUMBANI KWA
KINA ALICE
baba aliangalia kwenye darubini yake ya kichawi na akamkuta Alice yupo anakula ugali samaki na kelvin mzeealishtuka sana na kusema sabrina…….. kwa hasira
……..
Sabrina aliitika “abee baba “……
kwa hasira ” hiki nini sabrina mdogo wako anacheza na maadui zetu tena yupo ndani kwa mwanaume wanakula ugali samaki , vipi akikutana na kijana wa hovyo si atawekwa kwenye menu pia aje huku na mimi ya binadamu ……” mzee alikuwa kakasirika sana lakini hiyo
Sabrina alisema lakini baba…… mzee
alimstopisha kwa bonge la kofi ((paaàaaaaaaaaaaaaaaaaaah ) lakini nini
……
0 Comments